1. Kujibu kwa upole hutuliza hasira,lakini neno kali huchochea hasira.
2. Ulimi wa mwenye hekima hueneza maarifa,lakini watu wapumbavu hububujika upuuzi.
3. Macho ya Mwenyezi-Mungu huona kila kitu,humchunguza mtu mwema na mtu mbaya.
4. Ulimi mpole ni chanzo cha uhai,lakini uovu wake huvunja moyo.