Methali 14:32-35 Biblia Habari Njema (BHN)

32. Mwovu huangamizwa kwa matendo yake maovu,lakini mwadilifu hupata usalama kwa unyofu wake.

33. Hekima imo moyoni mwa mtu mwenye busara;haipatikani kamwe mioyoni mwa wapumbavu.

34. Uadilifu hukuza taifa,lakini dhambi ni balaa kwa taifa lolote.

35. Mfalme humfadhili mtumishi atendaye kwa hekima,lakini hasira yake huwakumba watendao yasiyofaa.

Methali 14