32. Mwovu huangamizwa kwa matendo yake maovu,lakini mwadilifu hupata usalama kwa unyofu wake.
33. Hekima imo moyoni mwa mtu mwenye busara;haipatikani kamwe mioyoni mwa wapumbavu.
34. Uadilifu hukuza taifa,lakini dhambi ni balaa kwa taifa lolote.
35. Mfalme humfadhili mtumishi atendaye kwa hekima,lakini hasira yake huwakumba watendao yasiyofaa.