15. Mjinga huamini kila kitu anachoambiwa,lakini mwenye busara huwa na tahadhari.
16. Mwenye hekima ni mwangalifu na huepa uovu,lakini mpumbavu hajizuii wala hana uangalifu.
17. Mwenye kuwaka hasira haraka hutenda kipumbavu,lakini mwenye busara ana uvumilivu.
18. Wajinga hurithi upumbavu,lakini wenye busara hutuzwa taji ya maarifa.
19. Waovu watapiga magoti mbele ya watu wema,watu wabaya mlangoni mwa waadilifu.