Methali 13:5-8 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Mwadilifu huuchukia uongo,lakini mwovu hutenda kwa aibu na fedheha.

6. Uadilifu huwalinda wenye mwenendo mnyofu,lakini dhambi huwaangusha waovu.

7. Baadhi hujidai kuwa matajiri kumbe hawana kitu;wengine hujiona kuwa maskini hali wana mali tele.

8. Fidia ya mtu ni mali yake,lakini maskini hana cha kutishwa.

Methali 13