22. Mtu mwema huwaachia urithi uzao wake,lakini mali ya mwenye dhambi imerundikiwa waadilifu.
23. Shamba la maskini hutoa mazao mengi,lakini bila haki hunyakuliwa.
24. Asiyemwadhibu mtoto wake hampendi;lakini ampendaye mwanawe humrudi mapema.
25. Mwadilifu anacho chakula cha kumtosheleza,lakini tumbo la waovu hutaabika kwa njaa.