Methali 13:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mtoto mwenye hekima husikia maagizo ya baba yake,lakini mwenye dharau hasikilizi maonyo.

2. Mtu mwema hupata mema kutokana na maneno yake,lakini wadanganyifu huishi kwa ukatili.

3. Achungaye mdomo wake huyahifadhi maisha yake,anayeropoka ovyo hujiletea maangamizi.

4. Mvivu hutamani lakini hapati chochote,hali mwenye bidii hujaliwa riziki kwa wingi.

5. Mwadilifu huuchukia uongo,lakini mwovu hutenda kwa aibu na fedheha.

Methali 13