18. Maneno ya ovyo hujeruhi kama upanga,lakini asemayo mwenye hekima huponesha kidonda.
19. Ukweli hudumu milele,lakini uongo ni wa kitambo tu.
20. Wanaopanga maovu wamejaa udanganyifu moyoni,lakini wanaonuia mema hupata furaha.
21. Waadilifu hawapatwi na jambo lolote baya,lakini waovu wamejaa dhiki.
22. Midomo isemayo uongo ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini watu waaminifu ni furaha yake.
23. Mwenye busara huficha maarifa yake,lakini wapumbavu hutangaza upumbavu wao.