8. Mtu mnyofu huokolewa katika shida,na mwovu huingia humo badala yake.
9. Asiyemcha Mungu huangamiza wengine kwa mdomo wake,lakini mwadilifu huokolewa kwa maarifa yake.
10. Waadilifu wakipata fanaka mji hushangilia,na waovu wakiangamia watu hupiga vigelegele.
11. Mji hufanikishwa kwa baraka za wanyofu,lakini huangamizwa kwa mdomo wa waovu.
12. Anayemdharau jirani yake hana akili,mtu mwenye busara hukaa kimya.
13. Apitapitaye akichongea hutoa siri,lakini anayeaminika rohoni huficha siri.