Methali 11:19-22 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Mtu anayepania kuwa mwadilifu ataishi,lakini anayechagua kutenda maovu atakufa.

20. Wenye nia mbaya ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu,lakini wenye mwenendo mwema ni furaha yake.

21. Hakika mwovu hataepa kuadhibiwa,lakini waadilifu wataokolewa.

22. Mwanamke mzuri asiye na akili,ni kama pete ya dhahabu puani mwa nguruwe.

Methali 11