26. Kama ilivyo siki kwa meno au moshi machoni,ndivyo alivyo mvivu kwa bwana wake.
27. Kumcha Mwenyezi-Mungu hurefusha maisha,lakini miaka ya waovu itakuwa mifupi.
28. Tumaini la mwadilifu huishia kwenye furaha,lakini tazamio la mwovu huishia patupu.
29. Mwenyezi-Mungu ni ngome ya wanyofu,lakini watendao maovu atawaangamiza.
30. Waadilifu kamwe hawataondolewa nchini,lakini waovu hawatakaa katika nchi.