Methali 10:26-30 Biblia Habari Njema (BHN)

26. Kama ilivyo siki kwa meno au moshi machoni,ndivyo alivyo mvivu kwa bwana wake.

27. Kumcha Mwenyezi-Mungu hurefusha maisha,lakini miaka ya waovu itakuwa mifupi.

28. Tumaini la mwadilifu huishia kwenye furaha,lakini tazamio la mwovu huishia patupu.

29. Mwenyezi-Mungu ni ngome ya wanyofu,lakini watendao maovu atawaangamiza.

30. Waadilifu kamwe hawataondolewa nchini,lakini waovu hawatakaa katika nchi.

Methali 10