Methali 1:18-25 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Wao huvizia na kujiangamiza wao wenyewe,hutega mtego wa kujinasa wao wenyewe.

19. Ndivyo zilivyo njia za waishio kwa ukatili;ukatili huyaangamiza maisha ya wakatili.

20. Hekima huita kwa sauti barabarani,hupaza sauti yake sokoni;

21. huita juu ya kuta,hutangaza penye malango ya mji:

22. “Enyi wajinga! Mpaka lini mtapenda kuwa wajinga?Mpaka lini wenye dharau watafurahia dharau zao,na wapumbavu kuchukia maarifa?

23. Sikilizeni maonyo yangu;nitawamiminia mawazo yangu,nitawajulisha maneno yangu.

24. Kwa kuwa nimewaita mkakataa kusikiliza,nimewapungia mkono mje mkakataa,

25. mkapuuza mashauri yangu yote,wala hamkuyajali maonyo yangu,

Methali 1