17. Mtego utegwao huku ndege anaona,mtego huo wategwa bure.
18. Wao huvizia na kujiangamiza wao wenyewe,hutega mtego wa kujinasa wao wenyewe.
19. Ndivyo zilivyo njia za waishio kwa ukatili;ukatili huyaangamiza maisha ya wakatili.
20. Hekima huita kwa sauti barabarani,hupaza sauti yake sokoni;
21. huita juu ya kuta,hutangaza penye malango ya mji:
22. “Enyi wajinga! Mpaka lini mtapenda kuwa wajinga?Mpaka lini wenye dharau watafurahia dharau zao,na wapumbavu kuchukia maarifa?
23. Sikilizeni maonyo yangu;nitawamiminia mawazo yangu,nitawajulisha maneno yangu.
24. Kwa kuwa nimewaita mkakataa kusikiliza,nimewapungia mkono mje mkakataa,
25. mkapuuza mashauri yangu yote,wala hamkuyajali maonyo yangu,