Mathayo 26:66-72 Biblia Habari Njema (BHN)

66. Nyinyi mwaonaje?” Wao wakamjibu, “Anastahili kufa!”

67. Kisha wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi. Wengine wakiwa wanampiga makofi,

68. wakasema, “Tubashirie basi, wewe Kristo; ni nani amekupiga!”

69. Petro alikuwa ameketi nje uani. Basi, mtumishi mmoja wa kike akamwendea, akasema, “Wewe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”

70. Petro akakana mbele ya wote akisema, “Sijui hata unasema nini.”

71. Alipokuwa akitoka mlangoni, mtumishi mwingine wa kike akamwona, akawaambia wale waliokuwa pale, “Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”

72. Petro akakana tena kwa kiapo: “Simjui mtu huyo.”

Mathayo 26