Mathayo 25:11-15 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Baadaye wale wasichana wengine wakaja, wakaita: ‘Bwana, Bwana, tufungulie!’

12. Lakini yeye akawajibu, ‘Nawaambieni kweli, siwajui nyinyi.’”

13. Kisha Yesu akasema, “Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.

14. “Wakati huo itakuwa kama mtu mmoja aliyetaka kusafiri ngambo: Aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake.

15. Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: Mmoja fedha talanta tano, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja, kisha akasafiri.

Mathayo 25