11. Baadaye wale wasichana wengine wakaja, wakaita: ‘Bwana, Bwana, tufungulie!’
12. Lakini yeye akawajibu, ‘Nawaambieni kweli, siwajui nyinyi.’”
13. Kisha Yesu akasema, “Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.
14. “Wakati huo itakuwa kama mtu mmoja aliyetaka kusafiri ngambo: Aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake.
15. Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: Mmoja fedha talanta tano, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja, kisha akasafiri.