Mathayo 24:41-44 Biblia Habari Njema (BHN)

41. Kina mama wawili watakuwa wanasaga nafaka, mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.

42. Basi, kesheni, kwa maana hamjui siku atakayokuja Bwana wenu.

43. Lakini kumbukeni jambo hili: Kama mwenye nyumba angejua siku mwizi atakapofika, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.

44. Kwa hiyo, nanyi pia muwe tayari, kwa maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”

Mathayo 24