38. Hii ndiyo amri kuu na ya kwanza.
39. Ya pili inafanana na hiyo: ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe’.
40. Sheria yote ya Mose na mafundisho ya manabii vinategemea amri hizi mbili.”
41. Mafarisayo walipokusanyika pamoja, Yesu aliwauliza,
42. “Nyinyi mwaonaje juu ya Kristo? Je, ni mwana wa nani?” Wakamjibu, “Wa Daudi.”
43. Yesu akawaambia, “Basi, inawezekanaje kwamba kwa nguvu ya Roho Mtakatifu Daudi anamwita yeye Bwana? Maana alisema: