Mathayo 22:20-24 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Basi, Yesu akawauliza, “Sura na chapa hii ni ya nani?”

21. Wakamjibu, “Ni ya Kaisari.” Hapo Yesu akawaambia, “Basi, ya Kaisari mpeni Kaisari, na ya Mungu mpeni Mungu.”

22. Waliposikia hivyo wakashangaa; wakamwacha, wakaenda zao.

23. Siku hiyo, baadhi ya Masadukayo wasemao wafu hawafufuki walimwendea Yesu.

24. Basi, wakamwambia, “Mwalimu, Mose alisema mtu aliyeoa akifa bila kuacha watoto, lazima ndugu yake amwoe huyo mama mjane, ili ampatie ndugu yake watoto.

Mathayo 22