Mathayo 17:20-23 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Yesu akawajibu, “Kwa sababu ya imani yenu haba. Nawaambieni kweli, kama tu mkiwa na imani, iwe ndogo hata kama mbegu ya haradali, mtaweza kuuambia mlima huu: ‘Toka hapa uende pale,’ nao utakwenda. Hakuna chochote ambacho hakingewezekana kwenu. [

21. Pepo wa namna hii hawezi kuondolewa ila kwa sala na kufunga.”]

22. Walipokuwa pamoja huko Galilaya, Yesu aliwaambia, “Mwana wa Mtu atakabidhiwa kwa watu.

23. Watamuua, lakini siku ya tatu atafufuliwa.” Wanafunzi wakahuzunika mno.

Mathayo 17