Mathayo 13:5-16 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Zikaota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.

6. Jua lilipochomoza, ziliteketea; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.

7. Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga.

8. Nyingine zilianguka penye udongo mzuri, zikaota, zikazaa: Nyingine punje mia, nyingine sitini na nyingine thelathini.

9. Mwenye masikio na asikie!”

10. Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwuliza, “Kwa nini unasema na watu kwa mifano?”

11. Yesu akawajibu, “Nyinyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, lakini wao hawakujaliwa.

12. Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa; lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.

13. Ndio maana ninasema nao kwa mifano, kwa sababu wanatazama lakini hawaoni, wanasikiliza lakini hawasikii, wala hawaelewi.

14. Kwao yametimia yale aliyosema nabii Isaya:‘Kusikia mtasikia, lakini hamtaelewa.Kutazama mtatazama, lakini hamtaona.

15. Maana akili za watu hawa zimepumbaa,wameyaziba masikio yao,wameyafumba macho yao.La sivyo, wangeona kwa macho yao,wangesikia kwa masikio yao,wangeelewa kwa akili zao,na kunigeukia, asema Bwana,nami ningewaponya.’

16. “Lakini heri yenu nyinyi, maana macho yenu yanaona na masikio yenu yanasikia.

Mathayo 13