Mathayo 12:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Au je, hamjasoma katika kitabu cha sheria kwamba kila siku ya Sabato makuhani huivunja sheria hekaluni, lakini hawafikiriwi kuwa na hatia?

6. Basi, nawaambieni kwamba hapa pana kikuu kuliko hekalu.

7. Kama tu mngejua maana ya maneno haya: ‘Nataka huruma wala si tambiko,’ hamngewahukumu watu wasio na hatia.

8. Maana Mwana wa Mtu ana uwezo juu ya Sabato.”

9. Yesu alitoka hapo, akaenda katika sunagogi lao.

Mathayo 12