9. Lakini, mlikwenda kuona nini? Nabii? Naam, hakika ni zaidi ya nabii.
10. “Huyu ndiye anayesemwa katika Maandiko Matakatifu:‘Tazama, mimi namtuma mjumbe wangu akutangulie,ambaye atakutayarishia njia yako’.
11. Kweli nawaambieni, miongoni mwa watoto wote wa watu, hajatokea aliye mkuu kuliko Yohane Mbatizaji. Hata hivyo, yule aliye mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni, ni mkubwa kuliko yeye.