6. Ila nendeni kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.
7. Mnapokwenda hubirini hivi: ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’
8. Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo. Mmepewa bure, toeni bure.
9. Msichukue mifukoni mwenu dhahabu, wala fedha, wala sarafu za shaba.
10. Msichukue mkoba wa kuombea njiani, wala koti la ziada, wala viatu, wala fimbo. Maana mfanyakazi anastahili riziki yake.
11. “Mkiingia katika mji wowote au kijiji, tafuteni humo mtu anayestahili kutembelewa, na kaeni huko mpaka mtakapoondoka mahali hapo.
12. Mnapoingia nyumbani wasalimuni wenyeji wake.
13. Kama wenyeji wa nyumba hiyo wanastahili salamu hiyo, basi, amani yenu itakaa pamoja nao. Lakini ikiwa hawastahili, basi amani yenu itawarudia nyinyi.