Mathayo 10:11-13 Biblia Habari Njema (BHN)

11. “Mkiingia katika mji wowote au kijiji, tafuteni humo mtu anayestahili kutembelewa, na kaeni huko mpaka mtakapoondoka mahali hapo.

12. Mnapoingia nyumbani wasalimuni wenyeji wake.

13. Kama wenyeji wa nyumba hiyo wanastahili salamu hiyo, basi, amani yenu itakaa pamoja nao. Lakini ikiwa hawastahili, basi amani yenu itawarudia nyinyi.

Mathayo 10