Matendo 2:26-29 Biblia Habari Njema (BHN)

26. Kwa hiyo, moyo wangu ulifurahi;tena nilipiga vigelegele vya furaha.Mwili wangu utakaa katika tumaini,

27. maana hutaiacha roho yangu kuzimu,wala kumruhusu mtakatifu wako aoze.

28. Umenionesha njia za uhai,umenijaza furaha kwa kuwako kwako!’

29. “Ndugu zangu, napenda kuwaambieni waziwazi juu ya mambo yaliyompata Daudi, babu yetu. Yeye alikufa, akazikwa, tena kaburi lake liko papa hapa petu mpaka leo.

Matendo 2