Matendo 2:17-19 Biblia Habari Njema (BHN)

17. ‘Katika siku zile za mwisho, asema Bwana,nitawamiminia binadamu wote Roho wangu.Watoto wenu wa kiume na wa kike watatoa unabii,vijana wenu wataona maono,na wazee wenu wataota ndoto.

18. Naam, hata watumishi wangu wa kiume na kike,nitawamiminia Roho wangu siku zile,nao watatoa unabii.

19. Nitatenda miujiza juu angani,na ishara chini duniani;kutakuwa na damu, moto na moshi mzito;

Matendo 2