46. Hata hivyo, Paulo na Barnaba waliongea kwa uhodari zaidi, wakasema, “Ilikuwa ni lazima neno la Mungu liwafikieni nyinyi kwanza; lakini kwa kuwa mmelikataa na kujiona hamstahili uhai wa milele, basi, tunawaacheni na kuwaendea watu wa mataifa mengine.
47. Maana Bwana alituagiza hivi:‘Nimekuweka wewe uwe mwanga kwa watu wa mataifa,ili uwaletee watu wokovu pote ulimwenguni.’”
48. Watu wa mataifa mengine waliposikia jambo hilo walifurahi, wakausifu ujumbe wa Mungu; na wale waliokuwa wamechaguliwa kupata uhai wa milele, wakawa waumini.
49. Neno la Bwana likaenea kila mahali katika sehemu ile.