Marko 8:7-13 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Walikuwa pia na visamaki vichache. Yesu akavibariki, akaamuru vigawiwe watu vilevile.

8. Watu wakala, wakashiba. Wakakusanya makombo wakajaza vikapu saba.

9. Nao waliokula walikuwa watu wapatao 4,000. Yesu akawaaga,

10. na mara akapanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akaenda wilaya ya Dalmanutha.

11. Mafarisayo walikuja, wakaanza kujadiliana na Yesu. Kwa kumjaribu, wakamtaka afanye ishara kutoka mbinguni.

12. Yesu akahuzunika rohoni, akasema, “Mbona kizazi hiki kinataka ishara? Kweli nawaambieni, kizazi hiki hakitapewa ishara yoyote.”

13. Basi, akawaacha, akapanda tena mashua, akaanza safari kwenda ngambo ya pili ya ziwa.

Marko 8