Marko 5:3-5 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Mtu huyo alikuwa akiishi makaburini wala hakuna mtu aliyeweza tena kumfunga kwa minyororo.

4. Mara nyingi walimfunga kwa pingu na minyororo lakini kila mara aliweza kuikata hiyo minyororo na kuzivunja hizo pingu, wala hakuna mtu aliyeweza kumzuia.

5. Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani akipaza sauti na kujikatakata kwa mawe.

Marko 5