56. Watu wengi walitoa ushahidi wa uongo juu ya Yesu, lakini ushahidi wao haukupatana.
57. Kisha wengine walisimama, wakatoa ushahidi wa uongo wakisema:
58. “Tulimsikia mtu huyu akisema, ‘Nitaliharibu hekalu hili lililojengwa kwa mikono, na kwa siku tatu nitajenga lingine lisilojengwa kwa mikono.’”
59. Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukupatana.