Marko 14:56-59 Biblia Habari Njema (BHN)

56. Watu wengi walitoa ushahidi wa uongo juu ya Yesu, lakini ushahidi wao haukupatana.

57. Kisha wengine walisimama, wakatoa ushahidi wa uongo wakisema:

58. “Tulimsikia mtu huyu akisema, ‘Nitaliharibu hekalu hili lililojengwa kwa mikono, na kwa siku tatu nitajenga lingine lisilojengwa kwa mikono.’”

59. Lakini hata hivyo, ushahidi wao haukupatana.

Marko 14