Marko 1:25-28 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Yesu akamkemea huyo pepo akisema, “Nyamaza! Mtoke mtu huyu.”

26. Basi, huyo pepo mchafu akamtikisatikisa mtu huyo, kisha akalia kwa sauti kubwa, akamtoka.

27. Watu wote wakashangaa, wakaulizana, “Ni mambo gani haya? Je, ni mafundisho mapya? Mtu huyu anayo mamlaka ya kuamuru hata pepo wachafu, nao wanamtii!”

28. Habari za Yesu zikaenea upesi kila mahali katika eneo la Galilaya.

Marko 1