Maombolezo 5:17-22 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Kwa ajili hiyo tumeugua moyoni,kwa mambo hayo macho yetu yamefifia.

18. Maana mlima Siyoni umeachwa tupu,mbweha wanazurura humo.

19. Lakini wewe Mwenyezi-Mungu watawala milele,utawala wako wadumu vizazi vyote.

20. Mbona umetuacha muda mrefu hivyo?Mbona umetutupa siku nyingi hivyo?

21. Uturekebishe ee Mwenyezi-Mungu, nasi tukurudie,uturudishie fahari yetu kama zamani.

22. Au, je, umetukataa kabisa?Je, umetukasirikia mno?

Maombolezo 5