3. Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani. Akawa anahubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
4. Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya:“Sauti ya mtu anaita jangwani:‘Mtayarishieni Bwana njia yake;nyosheni barabara zake.
5. Kila bonde litafukiwa,kila mlima na kilima vitasawazishwa;palipopindika patanyoshwa,njia mbaya zitatengenezwa.