Luka 23:29-32 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Maana, hakika siku zitakuja ambapo watasema: ‘Heri yao wale walio tasa, ambao hawakupata kuzaa wala kunyonyesha watoto!’

30. Wakati huo, ndipo watu wataanza kuiambia milima: ‘Tuangukieni!’ Na vilima, ‘Tufunikeni!’

31. Kwa maana, kama watu wanautendea mti mbichi namna hiyo, itakuwaje kwa mti mkavu?”

32. Waliwachukua pia watu wengine wawili, wahalifu, wauawe pamoja naye.

Luka 23