16. Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia.” [
17. Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.]
18. Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!” (
19. Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
20. Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
21. lakini wao wakapiga kelele: “Msulubishe, msulubishe!”
22. Pilato akawaambia mara ya tatu, “Amefanya ubaya gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie.”
23. Lakini wao wakazidi kupiga kelele kwa nguvu sana, kwamba Yesu ni lazima asulubiwe. Mwishowe, sauti zao zikashinda.
24. Basi, Pilato akaamua kwamba matakwa yao yatimizwe.