Luka 23:15-18 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.

16. Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia.” [

17. Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.]

18. Lakini wote wakapiga kelele pamoja: “Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!” (

Luka 23