Luka 21:28-33 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia.”

29. Kisha akawaambia mfano: “Angalieni mtini na miti mingine yote.

30. Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba majira ya mavuno yamekaribia.

31. Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.

32. Kweli nawaambieni, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.

33. Mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.

Luka 21