2. wakasema, “Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?”
3. Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:
4. Mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”
5. Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka kwa Mungu, yeye atatuuliza: ‘Mbona hamkumsadiki?’
6. Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”