Luka 20:2-6 Biblia Habari Njema (BHN)

2. wakasema, “Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?”

3. Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:

4. Mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”

5. Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka kwa Mungu, yeye atatuuliza: ‘Mbona hamkumsadiki?’

6. Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”

Luka 20