20. Tena akauliza: “Nitaulinganisha ufalme wa Mungu na nini?
21. Ni kama chachu aliyoitwaa mama mmoja na kuichanganya pamoja na unga madebe mawili na nusu kisha unga wote ukaumuka.”
22. Yesu aliendelea na safari yake kwenda Yerusalemu huku akipitia mijini na vijijini, akihubiri.
23. Mtu mmoja akamwuliza, “Je, Mwalimu, watu watakaookoka ni wachache?”
24. Yesu akawaambia, “Jitahidini kuingia kwa kupitia mlango mwembamba; maana nawaambieni, wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza.