Kutoka 6:27-30 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Ndio haohao Mose na Aroni walioongea na Farao, mfalme wa Misri, juu ya kuwatoa Waisraeli nchini Misri.

28. Siku ile Mwenyezi-Mungu alipoongea na Mose nchini Misri,

29. alimwambia, “Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu. Mwambie Farao, mfalme wa Misri, maneno yote ninayokuambia.”

30. Lakini Mose akamwambia Mwenyezi-Mungu, “Mimi sina ufasaha wa kuongea; Farao atanisikilizaje?”

Kutoka 6