Kutoka 40:21-28 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Kisha akaliweka lile sanduku la maamuzi ndani ya hema na kutundika pazia, na kwa namna hiyo akalisitiri sanduku la maamuzi, kama alivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu.

22. Aliweka meza ndani ya hema la mkutano, upande wa kaskazini, sehemu ya nje ya pazia,

23. na juu yake akaipanga mikate iliyotolewa kwa Mwenyezi-Mungu, kama alivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu.

24. Alikiweka kinara ndani ya hema la mkutano, upande wa kusini, mkabala wa meza.

25. Humo, mbele ya Mwenyezi-Mungu, akaziwasha taa zake, kama alivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu.

26. Aliiweka ile madhabahu ya dhahabu katika hema, mbele ya pazia,

27. na kufukiza ubani wenye harufu nzuri juu yake, kama alivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu.

28. Alitundika pazia kwenye mlango wa hema takatifu,

Kutoka 40