19. Kisha alitengeneza kifuniko cha ngozi laini ya kondoo dume, na juu yake kifuniko kingine cha ngozi laini ya mbuzi.
20. Halafu akalitengenezea hema mbao za mjohoro za kusimama wima.
21. Kila ubao ulikuwa na urefu wa mita 4 na upana wa sentimita 66.
22. Kila ubao ulikuwa na ndimi mbili za kuunganishia. Mbao zote za hema alizifanyia ndimi.
23. Mbao hizo za hema zilitengenezwa hivi: Mbao ishirini upande wa kusini,