1. Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose,
2. “Mimi nimemteua Bezaleli, mwana wa Uri, mjukuu wa Huri, wa kabila la Yuda
3. na kumjaza roho wangu. Nimempatia uzoefu na akili, maarifa na ufundi,
4. ili abuni kazi za usanii na kufanya kazi za kufua dhahabu, fedha na shaba.