Kutoka 30:3-5 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Yote utaipaka dhahabu safi: Upande wake wa juu, pande zake zote za ubavuni na pembe zake; pia utaizungushia ukingo wa dhahabu.

4. Utaitengenezea pete mbili za dhahabu na kuzitia chini ya ukingo wake kwenye pande mbili zinazokabiliana; hizo pete zitatumiwa kushikilia mipiko wakati wa kuibeba.

5. Mipiko hiyo iwe ya mjohoro na ipakwe dhahabu.

Kutoka 30