Kutoka 26:30-32 Biblia Habari Njema (BHN)

30. Hivyo utalitengeneza hema hilo kulingana na mfano niliokuonesha mlimani.

31. “Utatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu na kitani safi iliyosokotwa. Pazia hilo utalitarizi kwa ustadi kwa viumbe wenye mabawa.

32. Utalitundika pazia kwenye nguzo nne za mjohoro zilizopakwa dhahabu, zenye kulabu za dhahabu na vikalio vinne vya fedha.

Kutoka 26