Kutoka 25:38-40 Biblia Habari Njema (BHN)

38. Tengeneza pia koleo zake na visahani vyake kwa dhahabu safi.

39. Utatumia kilo thelathini na tano za dhahabu safi kutengeneza kinara hicho na vifaa vyake.

40. Hakikisha kwamba umevitengeneza kwa mfano uliooneshwa kule mlimani.

Kutoka 25