Kutoka 25:12-16 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Kisha utalitengenezea pete nne na kuzitia miguuni pake, kila mguu pete moja.

13. Utatengeneza mipiko ya mjohoro na kuipaka dhahabu.

14. Mipiko hiyo utaipitisha katika pete zilizo pande mbili za sanduku, kwa ajili ya kulibebea.

15. Mipiko hiyo itabaki daima katika pete; isitolewe wakati wowote.

16. Ndani ya sanduku hilo utaweka vibao viwili vya mawe vya ushuhuda.

Kutoka 25