Kutoka 25:10-13 Biblia Habari Njema (BHN)

10. “Waisraeli watengeneze sanduku la mbao za mjohoro, lenye urefu wa sentimita 110, upana sentimita 66, na kimo sentimita 66.

11. Utalipaka sanduku hilo dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu pande zote.

12. Kisha utalitengenezea pete nne na kuzitia miguuni pake, kila mguu pete moja.

13. Utatengeneza mipiko ya mjohoro na kuipaka dhahabu.

Kutoka 25