Kutoka 22:15-24 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Lakini kama mwenyewe alikuwako, basi aliyemwazima hatalipa chochote. Kama alikuwa ni mnyama aliyekodishwa, mwenyewe ataikubali tu bei ya kukodisha.

16. “Mtu akimshawishi bikira ambaye hajaposwa, akalala naye, lazima atoe mahari na kumwoa msichana huyo.

17. Baba wa huyo msichana akikataa katakata kumwoza binti yake, mtu huyo atalipa fedha ya mahari inayostahili msichana aliye bikira.

18. “Usimwache mwanamke mchawi aishi.

19. “Anayezini na mnyama lazima auawe.

20. “Anayemtolea tambiko mungu mwingine badala ya Mwenyezi-Mungu pekee, lazima aangamizwe kabisa.

21. “Msimdhulumu mgeni wala kumtesa, maana nanyi pia mlikuwa wageni nchini Misri.

22. Msimtese mjane au yatima.

23. Kama mkiwadhulumu hao nao wakanililia, hakika nitakisikiliza kilio chao,

24. na hasira yangu itawaka, nami nitawaueni kwa upanga, na wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu yatima.

Kutoka 22