Kutoka 20:20-23 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Mose akawaambia, “Msiogope, maana Mungu amekuja kuwajaribu ili mpate kumcha yeye daima na msitende dhambi.”

21. Watu wote walisimama mbali wakati Mose alipokaribia lile wingu zito alimokuwamo Mungu.

22. Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli: ‘Mmejionea nyinyi wenyewe kwamba nimeongea nanyi kutoka mbinguni.

23. Mtaniheshimu mimi peke yangu wala msijifanyie miungu ya fedha wala ya dhahabu.

Kutoka 20