5. Vilindi vya maji vimewafunika,wameporomoka baharini kama jiwe.
6. “Mkono wako wa kulia ee Mwenyezi-Mungu watukuka kwa nguvu;kwa mkono wako wa kulia ee Mwenyezi-Mungu wawaponda adui.
7. Kwa wingi wa ukuu wako wawaangamiza wapinzani wako;wawapulizia ghadhabu yako nayo yawateketeza kama makapi.
8. Kwa pumzi ya pua yako maji yalirundikana,mawimbi yakasimama wima kama ukuta;vilindi katikati ya bahari vikagandamana.