Kutoka 15:5-8 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Vilindi vya maji vimewafunika,wameporomoka baharini kama jiwe.

6. “Mkono wako wa kulia ee Mwenyezi-Mungu watukuka kwa nguvu;kwa mkono wako wa kulia ee Mwenyezi-Mungu wawaponda adui.

7. Kwa wingi wa ukuu wako wawaangamiza wapinzani wako;wawapulizia ghadhabu yako nayo yawateketeza kama makapi.

8. Kwa pumzi ya pua yako maji yalirundikana,mawimbi yakasimama wima kama ukuta;vilindi katikati ya bahari vikagandamana.

Kutoka 15